A-Z Maisha ya PATRICK, Aliyoyapitia Hadi Kufa!

  • 6 years ago
A-Z Maisha ya PATRICK, Aliyoyapitia Hadi Kufa!

Patrick Peter, alizaliwa tarehe 17 mwezi wa 12 mwaka 2010 alikuwa ni mtoto wa taifa.

Nyota yake ilikuwa imeanza kung’aa mapema, kiasi kwamba watu mbalimbali pamoja na makampuni yakaanza kumtumia kwenye matangazo na filamu tofauti.

Lakini nyota yake imezimika ghafla kwenye dunia yetu hii ya mwili wa nyama.

Mtoto Patrick alikuwa akimpenda sana mungu hata kupelekea kubadilisha kabisa historia ya mama yake na kumtaka mama yake kuokoka na kuanza kusali ili kukaa mbali na mambo ya kidunia
Kuwa karibu sana na mungu kulifanya mtoto huyu kupenda sana kuimba nyimbo ambazo zimekuwa zikiimbwa na wasanii mbali mbali wa nyimbo za injili kitu kinacho waumiza sana watu wengi wanapoona video za mtoto huyu ambaye kifo chake kimegusa mioyo ya watu wengi.

Hata hivyo kuondoka kwa Patrick kunaacha funzo kubwa kwa kila mmoja wetu, kwa namna ambavyo mtoto anaweza kubadilisha maisha ya mzazi, kuleta upendo baina ya watu na hata kuunganisha jamii kwa jumla.

Patrick alianza kuugua ghafra na kutokana na mahojiano baadhi ambayo mama ake aliwahi kufanya enzi za uhai wa partrick alieleza hivi ,Tuliamka siku moja akawa hatembei Anatambaa tu.

Nilijua anatania lakini hali ikaendelea kuwa siriasi, Nikampeleka Hospitali ya Agha Khan, akafanyiwa vipimo nikaelezwa ana maumivu tu baadaye atakuwa sawa Lakini bado hakupona.

Install GlobalPublishersApp Android: iOS: Subscribe FACEBOOK: ... TWITTER: Visit

, Subscribe Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… /c/uwazi1 WEBSITE: FACEBOOK:

... TWITTER: INSTAGRAM: ..

Recommended