Magufuli Acha Machozi Ya Mamba! Amani TZ Unaiharibu wewe Period!

  • 6 years ago
Napenda Nijibu Hila na Hadaa za magufuli, Anadai Mikutano na Maandamano Vinaharibu amani, Mbona Yakweke anafanya? Mbona polepole akifanya Amani haiharibiki? Ujinga Mtupu. Tanzania amani haitavujwa kwa Mikutano ya Siasa au maandamano ya Watu Kuonyesha Kero zao! Amani Tanzania Inatishiwa na 1)Kukamatwa hovyo kwa Wabunge, 2)Kupiga watu Risasi eg, Tundu Lissu, Akwilina na Wale Polisi wa Bank na Vikindu (Muulizeni Sirro) 3) Kutekwa na Kupotezwa Watu/Wanasiasa/ 4) Kuvunjia watu Makazi na Mali zao kwa Upendeleo 5) Kuzuia Matangazo ya Moja kwa Moja Bungeni Lakini wewe Ukihutubia Bungeni Unataka yawe Live! 6) Kuiba Pesa za Walipa kodi na Kuzitumia kirushwa Kununua Viongozi wa Upinzani, Kisha Kutumia Mamluki kusimamia chaguzi, Kutumia Polisi kupiga na Kuua na Kutisha watu ili kuiba Kura. Haya na Mengine Ndio hasa yatakayoharibu amani Tanzania kama hayajaiharibu Tayari. Unayosema wewe Ni Unafiki na Utumbo Mtupu.